Menyu

Kiswahili

Utamaduni mpya ulijitokeza uliokuwa Kiafrika na Kiislamu ukajielewa kuwa sehemu ya dunia ya Uislamu.

SWAHILI HUB

BLOGU YA KISWAHILI KWA AJILI YA KUSAFISHA FIKRA ZA WAAFRIKA!

DUNIYA MTI MKAVU

Kiumbe siulemee kamwe... Likuondokealo, lina heri nawe.

CHINI YA SHAMSHI

Mjomba'ngu Shamshi Kuzaliwa kwangu kulifululizwa na majonzi yas’o kuwa na mfano. Hili si ada kwa wana wengi duniani. Na kama ilivyokuwa kawaida katika jamii za kwetu Raha, waliniona mwenye shari hivyo kunipa jina Tabu. Japo haya si kuyanga’mua papo kwa hapo, niliyafahamu mtuo kwa mtuo kadri miaka ilivyozidi kuporomok...

Said Ahmed Mohammed

Uamuzi wa kuchagua hadithi zilizoandikwa kwa Kiengereza kufasiriwa kwa Kiswahili, ulitokana na Macmillan wenyewe. Nao walizichagua hadithi hizo kwa ubora wa hadithi zenyewe na umaarufu wa waandishi wenyewe.

Swahili Hub

PENDO LA SIRI. [23/05/2012]


PENDO LA SIRI.
[23/05/2012]
Hayo ya hayawi hayawi, yaliniangukia kama nanga. Kiza kilichojimwaya kati ya upenyu wa mwanga katika aushi yangu. Yapo niliyoyaamini; Anenae kuwa pendo, si faida ni uvundo. Huyo yu katika mwendo, wa ujinga na ubaya. Na'mi kwa ari ambayo sikufahamu mwanzo wake, nikatii amri yakuwa tupendaneni, tusitendeyane ubaya...

Ama kwa hakika yalianza kama mchezo. Mara 'My son', mara wavutia mara sijui nini:- almuradi niliungulika na mengine kuyatia asali bandia. Nikajitia upofu kwa dhana kuwa mapenzi ya mtandaoni