Menyu

Swahili Hub

Umuhimu Wa Maisha ya Binadamu




Wajibu wa dini yoyote ni kuwaongoza  binadamu kudumisha maadili fulani mema ili 
iwezekane kuishi maisha ya amani na kudumisha hadhi ya binadamu. Ama sivyo itakuwa
haiwezekani sisi kama binadamu kudai kuwa ni bora kuliko viumbe wengine, ambao
lengo lao la kuishi ni kupata tu chakula, makazi na ngono, Kama binadamu pia
wanatumia maisha yao kuzikidhi tu hizi haja za msingi, tutakuwa hatuna kitu chochote
cha zaidi cha kututofautisha kama wanadamu. Binadamu wamevuka maisha ya kujitahidi
kudumu tu na wanao uwezo wa kuchukua hatima ya maisha yao mikononi mwao.
Katika Ubudha tunaita hii Dharma. Viumbe wengine wanaoishi hawawezi kuifikia hii
Dharma  kwa  sababu  akili  ya  binadamu  ni  ya  juu  zaidi  kuliko  viumbe  wote
wengine  wanaoishi  katika  mbingu,  Ni akili  ya  binadamu  tu ndio inaweza  kuielewa
Dharma...  Inafaa  kukumbuka  kwamba  binadamu  ndio  pekee  katika  viumbe  wote
wanaoishi  katika  mbingu  ambao  wanaoweza  kubuni  mfumo  mgumu  wa dini.  Hata
Devas  na Brahmas  hawana  dini  yoyote  maalum.

Ingawa  tunawaabubu  deva(watu wanaokufa baada ya kuishi maisha ya thawabu
duniani)  na  brahmas(wakazi wa brahma loka,yaani ulimwengu wanakoishi watu wote
waliokufa duniani)  na  kutoa   sadaka   kwa  majina  yao,  ni  lazima  tukumbuke
kwamba  akili  yetu  ya  kibinadamu   ni  ya  juu   kuliko  yao.  Ndiyo  maana  deva  na
brahmas   hawawezi  kuwa  Budha.  Ni  binadamu  tu  ndiye  anayeweza  kuufikia
ufahamu  wa  juu  kabisa  kwa  sababu  ni  yeye  pekee  ndiye  anayeweza kuiendeleza
akili  yake  kufikia  kiwango  cha  juu  kabisa.

Baada  ya  kupewa  hii  akili  binadamu  anajitahidi  kuelewa  hali  halisi  ya  kuishi
kwake  na  kuunda  kanuni  zinazofaa  za  tabia  ambazo zitamfanya  atukuke  na  astahili
heshima,    Watu    wafikiriaji  ,  wa    kale    na    wa    sasa  ,  wametafakari    kwa    kina    sana  
kuhusu  maswali  matatu  ya  maisha  “  Mimi  ni  nani  ?”  “ Nafanya  nini  hapa ?”  “
Nahitajika ? “Majibu  ya  maswali  haya yanaweza  kutupa  msingi  wa  kuishi  maisha
yenye  maana..  Tunaiita hii  ndiyo  misingi  ya  maisha.

Misingi  ya  kuwa  binadamu  ni  ipi ?  Kulijibu  hili  swali  kwanza  inabidi  tujiulize
neno  ‘ binadamu ‘  mana  yake  nini,  Lugha  za  Pali  na  Sanskrit.zinatumia  neno ‘
manussa ‘  au  ‘ manusya ‘ kumaanisha  binadamu,  Ni neno  lenye  maana  sana,  Pia
neno  la  kuingereza  ‘ man ‘  linatokana  na  neno  la  kisanskrit  ‘ manu ‘
linalomaanisha  ‘  kufikiri ‘ . Binadamu  ndio  viumbe   pekee   wanaoweza  kuipalilia  na  kuiendeleza  akili  kufikia

kikomo    chake    cha    mwisho    kabisa.    Kiumbe      kama    huyo    anaitwa    manussa    (
binadamu ) . Neno ‘ man ‘ pia linatokana  na  neno  ‘  mana ‘  linalomaanisha ‘ akili ‘.
kwa  hiyo  yule  mwenye   akili  ya  kufikiri  anaitwa  mtu. Na  akili  yake  ya  juu  mtu
anaweza  kuziongoza  na  kuzielekeza  hamu  zake  na  anaweza  kuyatengeneza  maisha
yake  anavyochagua.

Wachina  wanamwita  binadamu ‘ yule  ambaye  ana  moyo  ambao  uko  tayari   kutenda
wema.’  Katika  moyo  wa  binadamu  lazima  kuwepo  huruma  na  kweli .. Kama
mambo  haya  mawili  hayapo  basi  mtu  hawezi  kufikirika  kwamba  ni  mtu  kweli,
Wanafalsafa  wa  magharibi  wanamwita  mtu  yule tu ambaye  anafikiri  kwa  kutumia
mantiki..  Binadamu  ndio  viumbe  pekee  wenye  mantiki  katika  vitendo  vyao.
Viumbe  wengine   wanategemea  hisia  tu  kuhakikisha  uwezo  wao  wa  kumudu
maisha,  kustarehe  na  kujilinda. Akili  ikipaliliwa  kwa  kuacha  mawazo  maovu  na
kuendeleza  thawabu  nzuri  mtu  anaweza  kuifikia  hii  shwari  ambayo  inaleta
kutakasika  kwa  akili.

HALI  YA  AKILI  YA  BINADAMU
Akili  ya   binadamu   inaweza  kupenyeza  na  kuchambua  elements  au  miundo  ya
dunia  katika  mbingu  yote.  Akili inaundwa  na  mawazo  yasiyodumu  ambayo
yanaibuka  na  kufifia  upesi  kama  umeme.  Kuna  nishati  nyingi  sana  katika  akili.
Hakuna  nishati  ambayo  inaweza  kulingana  na  akili  ya  binadamu,  Akili  ndio
mtangulizi  wa  kila  kitu,  akili  ndio  inayoongoza  na  vitu  vyote  vinavyo  chanzo
chake  katika  akili..  Budha  amesema  , ‘ Siifahamu  nishati  nyingine  kubwa  kuliko
akili  ya  binadamu  ambayo  inaweza  kukimbia  mbio sana,. Kwa  mfano  wale  ambao
wamesoma  sayansi  wanaweza  kuelewa  mara  moja  umbile  la  atom.  Atom
inabadilika  mara  milioni  chache  katika  muda  wa  nukta  moja.

Katika  saikolojia  ya  kibudha,  tunaambiwa  kwamba  kila  mara  akili  inapobadilika
mara  17 ,  mwili   unabadilika  mara  moja  tu.  Atom  na  element  pia  zinafanya  kazi
kwa  msingi  huo  huo.  Wale  ambao  wamesoma  baolojia  wanaweza  kuelewa
kwamba    chembe    chembe    za    uhai    (cells  )  na    kila    kitu    katika    mwili    wetu
kinabadilika  baada  ya  muda.  Nguvu   yetu  ya  akili  inaibuka  na  kutoweka  upesi
mara  elfu  moja  zaidi  kuliko  umeme.  Hivyo  ndivyo  ilivyo  akili.
Zaidi ya hayo .akili ndio inayosababisha kila kitu kinachotokea duniani .Budha anasema ‘
‘ ‘Akili  ndio  imesababisha  kila  kitu , kizuri  au  kibaya  kilichopo  katika  mbingu
yote’. Hivi  tulivyo  ni  matokeo  ya  yale  tuliyofikiri.

Ni  kwa  ajili  ya  taaswira  zetu  zilizopotoka  ndio  tunamlaumu  mungu,  majini  na
mashetani  kwa  matatizo  yetu.  Watu  wengine  wanaamini  kwamba  mateso  yetu  ya
leo   yamesababishwa  na  dhambi  ya  asili  iliyotendwa  na  babu  yetu  wa  kwanza
maelfu  ya   miaka  iliyopita.  Kama  ni  hivyo,  mateso  ya  wanyama  yanasabishwa  na
nini ?  Wao  pia  wanateseka  kutokana  na  ugonjwa, kuzeeka, na  kifo.  Nao  pia
wanateseka  kwa  ajili  ya  dhambi  ya  asili ? Mimea  pia  inateseka  kutokana  na  kuugua,  kuzeeka  na  kufa. Nayo  pia  inapata  matatizo  haya kwa  ajili  ya  dhambi  yao
ya  asili ?

Hakuna  mtu  anayeweweza  kuimiliki  akili  ya  mwingine,  lakini  kama  mtu
akiiendeleza  akili  yake mwenyewe,  basi  anaweza  kuwa  na  taathira  kubwa  sana,
kwa  wema  na  hata  pia  kwa  ubaya, kwa akili ya mwingine.  Maendeleo  ya  elimu  ya  
sayansi  yanaweza  kutumika  vizuri  au  vibaya  na  watu    kwa  sababu  zao za  ubinafsi.
Kwa  upande  mwingine,  akili  inaweza  kumilikiwa  na  kutumika  kuitathmini  na
kuielewa  Dharma  na  jinsi  mbingu  inavyofanya  kazi.

Kwa  kuiendeleza  akili  watu,  kwa  mfano,  wamegundua nguvu  iliyopo  ndani  ya
atom  na  wameitumia elimu  hii  kufanya  kazi  nyingi  zenye  manufaa.  Kinyume
chake,  katika  huu  utafiti  wa  atom  pia  wamevumbua   silaha  za  nyuklia  ambazo
zinaweza  kuiangamiza  dunia  yote.  Kama  akili  isipomilikiwa  na  kuzoezwa  kwa
usahihi,  hatari  zinazoweza  kufuatia  zitakuwa  hazitaswiriki, Mfano mmoja  unaokuja
akilini  haraka  ni  jinsi  Hitler  alivyotumia  akili  zake  nyingi  kwa  nia  za  uovu.
Karibu  aina  zote  nyingine  za  viumbe    zinatoweka  polepole  kutokana  na  hamu  za
kibinafsi  za  binadamu  kunakosababishwa  na  akili  ambazo  hazijazoezwa  kwa
usahihi. Wanachafua  maji  na  hewa  na  kuharibu  mazingara  huku  wakidai
wanayaendeleza, kumbe  ukweli  ni  kwamba  wanalenga  kuleta  uharibifu  tu.  Lazima
tukubali  kwamba  viumbe  wengine    hawaharibu  kitu  chochote katika mazingara  kwa
kiwango  kile  kile  ambacho  binadamu  wanafanya.

HALI  TATU  ZA  MAISHA  YA  BINADAMU
Kama  binadamu  tunazo  hali tatu.  au  tabia  tatu  ,yaani  hali  ya  unyama  ,hali  ya
binadamu  na  hali  ya  utakatifu  ..Siyo  lazima  tusubiri  kuzaliwa  mbinguni  au  motoni
ili  kuishi  mojawapo  ya  hali  hizi  .Wanyama  wanao  uwezo  mdogo  wa  kufikiri
lakini  kwa  kutumia  akili  yetu  ,binadamu  tunaweza  kuzithibiti  au  kuzimiliki  tabia
zetu  za  kinyama  na  kwa  kufanya  hivyo  tunaiendeleza  tabia  yetu  ya  kibinadamu  na
tunaweza  pia  kugundua  tabia  ya  kiroho  ndani  mwetu
 .
Wanyama  hawana  njia  za  kuzimiliki  tabia  zao  za  kinyama  kwa  sababu
wanatawaliwa   zaidi  na  hisia  tu  .Lakini  tukiwa  kama  binadamu  ,kwa  kutumia  akili
zetu  kuchambua  na  kufikiri  ,tumeelewa  mambo  mengine  ni  sawa  na mambo
mengine  siyo sawa ,kwamba  mambo    mengine  ni  ya  kidhalimu  na ni  ya  hatari  ,na
kwamba  mambo  mengine  ni  mazuri  na  yenye  faida  si  kwetu  sisi tu, bali  hata  kwa
wengine  pia .  Hii  ndiyo  maana binadamu  wamewekwa  kwenye  ngazi   ya  juu  zaidi
kuliko  viumbe  wengine  .

Kwa  kuithibiti  tabia  yetu  ya  kinyama ,kwa kuacha unyang’anyi au uporaji,na  kwa
kuendeleza  urafiki  na  huruma ,tunaendeleza   subira  ,uvumilivu   ,maelewano,  umoja
na  ushirikiano  na  nia  njema  .Hizi  ni  tabia  za  kiutu  . Lengo  la  msingi  la  dini ni kuzihimiza  na kuzikuza  hizi  tabia  .Lakini , lazima
tuelewe  kwamba  baadhi  ya  hizi  tabia  zimo  ndani  mwetu  .Tulikuwa  tumeziendeleza
baadhi  ya  hizi  tabia  njema  hata  kabla  ya  dini  kutokea .  .Akili  ya  binadamu
imeendelea  sana   kiasi  kwamba  inaweza  kwa  urahisi  kuzoezwa  ili  kufurahia
starehe  za  mbinguni .Viumbe wengine    hawawezi  kufanya  hivi ? . Akili  ya
binadamu  imetengenezwa  kwa  ustadi sana . Inaweza  kuunda  maisha  mabaya  ya
motoni.  Tofauti  na  viumbe  wengine  ambao  wanaua  kwa kujikinga  au  kwa  kupata
chakula, akili  inaweza  kumfanya  mtu  aue  kwa  tamaa,  kwa  husuda  au hata  kwa
kujifurahisha  tu.  Na  bado  hatosheki  mara  tu  anapotimiza  haja  moja,  hapo hapo
anakuwa  na  uchu  wa  kupata  kitu  kingine , matokeo  yake  anakuwa  kila  wakati
hana  furaha.

Mahatma  Gandhi  amesema, ‘ Dunia  inatosha  kwa  mahitaji  ya  kila  mtu,  lakini
haitoshi  kwa  tamaa  ya  mtu  mmoja  tu.’  Binadamu  wanapigana  wenyewe  kwa  ajili
ya  ule  uchu  wa  ajabu  wa  kutaka  kuwa  na  cheo  zaidi,  mamlaka  zaidi , pamoja  na
anasa  zaidi.

AINA  NNE  ZA  DINI
Zipo aina  nne   za  dini  katika  dunia  hii,  nazo  ni  dini ya asili, ya  oganaizesheni,  ya
ufunuo,  na dini iliyowekwa  katika  mfumo  wa  maisha.

1. DINI  YA  ASILI
Katika  siku  za  zamani,  zama  za zama,  binadamu  aliishi  kwa  woga  kwa  sababu
alikuwa  amezungukwa  na  mambo  ambayo  alishindwa  kuyaelewa.  Kwa hiyo akawa
anayaogopa  yale  mambo  ambayo  alishindwa  kuyaelewa.  Woga  unawafika  wale
ambao  wanashindwa  kuzielewa  sheria  za  maumbile.  Vitu  vinavyotisha  ni  hali  tu
za  akili;  yule  mtu  wa  kale  aliposhindwa  kuyaelewa  maumbile  na  ukweli  kuhusu
matukio  katika mazingara yake,  akaanza  kuamini  kwamba  kuna  nguvu  ya  uchawi
inayosabisha  haya  mambo  aliyokuwa  anashindwa  kuyaelewa , kama  vile  mabadiliko
ya  hali  ya  hewa,  kupatwa  kwa  jua,  radi,  ngurumo, mvua,  upinde  wa  mvua,
volcano,  mafuriko,  ukame  na  mambo  mengine  mengi. Alifikiri  kwamba
yanasababishwa  kichawi  na  nguvu  fulani,  na  kwamba  alikuwa  anahitajika  kutoa
sadaka  kuondoa  hasira  zao  ili  aweze  kuishi  kwa  amani.  Kwa  hiyo  akaanza
kuiabudu  na  kuomba  msaada   wao ili  aweze  kuyamudu  maisha  na  kupata  nguvu
dhidi  ya  wengine.  Baada  ya  muda  vitendo  na  imani  hizi  vikawa  mwanzo  wa
tambiko  na  sala,  ndio  ikanza  tunaichota  dini  ya  asili.

2. DINI  ILIYOUNDWA  KWA  OGANAIZESHENI  
Kabla  dini  hazijaanza,  watu  walikuwa  nayo  mawazo  ya  kibinadamu,  lakini  ‘ dini ‘
hasa  hazikuwepo. Kwa  kuziendeleza  tabia  zilizokuwepo  katika  nafsi  zao  za
ubinadamu  na  thawabu,  wakaanza  oganaizesheni  ya  matendo  fulani  na  kufuatana
na  jinsi  walivyofikiria  wakaunda  kanuni  za  tabia  kuiongoza  jamii  waliyokuwa
wanaishi. Nguvu  ya  aibu  na  woga (hiri na  ottappa )  ndio  mambo  yaliyowaongoza  na  kuamua  tabia  yao  kuhusu  wenyewe  pamoja  na  wengine  na  imani
zikaendelezwa  na  hatimaye  zikawa  dini.

3 DINI  YA  UFUNUO
Inatokana  na   mafundisho  yanayoletwa  na  mungu  mkuu  kupitia  mesenja  au  nabii
katika  mfumo  wa  amri  au  kanuni  za  dini.  Wafuasi  wanaamini  kwa  dhati  kwamba
mafundisho  wanayoyapata  ndio  msingi  wa  tabia  yao  ya  kiroho  na  katika  jamii.

4 DINI  ILIYOINGIZWA  KATIKA  MFUMO  WA  MAISHA
Katika  jamii  nyingine,  binadamu  wanaishi  maisha  ya  kidini  kwa  kuipenyeza  dini
katika  saikolojia,  falsafa,  katika  vyama  vya  siasa,  katika  shule,  na katika maadili
yao  kwa  utaratibu  mzuri.  Ili  kudumisha  amani  na  tabia  njema  wametunga kanuni
kuzikuza  tabia  za  kiutu,na kuishi kwa amani na kuyatanzua matatizo yao mengi ,na ili
waweze kuziondoa balaa na vurugu zinazotokea katika maisha.   Hizi  kanuni
zikihalalishwa  na  kupewa  msingi  wa  kiroho,  ndio  inasemekana  kwamba  dini
imeingia  katika  mfuma  wa  maisha.

Mtaalamu  maarufu  wa  kibuddha.  Bhikkhu  Budhadasa  anazipanga  dini  kwa  njia  
ifuatayo. 
•  Dini  ya  nguvu  za  muijiza  na  uchawi  ambayo  msingi  ni  woga  wa  wafuasi  
wake. 
•  Dini  ya  Imani – ambayo  tu  msingi  ni  imani  na  sala  . 
•  Dini  ya  Karma -  msingi  ni mtu  kujisaidia  ,  kujitegemea   
•  Dini  ya  Hekima  -msingi wake  ni  kufikiri  kwa  uhuru  .  
*    Dini  ya Amani   - Msingi  wake  ni  kutojidhuru  mwenyewe   au  wengine  
•  Dini  ya  upendo _ msingi  wake  ni  kutoa  vyote  au  kila  kitu  kwa  wengine 

MAANA  YA  UBUDHA  NA  DHARMA
Ubudha  lakini  haupo  katika  makundi  hayo  manne.  Kwa  sababu  ingawa  tunalitumia
neno  ‘dini’ kuuuita  Ubudha  tunaona  vigumu  kuuuita  Ubudha ‘ dini ‘ kufuatana  na
maana ya  hilo  neno  kama  inavyotolewa  katika  kamusi.  Kwa  mfano,  kamusi  ya
oxford  inaelezea  dini  kama “ muundo  wa  imani  na  kuabudu,  pamoja  na  binadamu
kutambua  kwamba  ipo  nguvu  kubwa  kuliko  binadamu  inayoongoza,  na  hasa
mungu  ambaye   anapaswa  kutiiwa.”  Neno  zuri  kupita  yote  ambalo  tunaweza
kulitumia  kuyaita  kwa  usahihi  mafundisho  ya  Budha  ni  ‘Dharma’  Kwa  ajili  neno
‘dini’  ndilo  limezoeleka,  kwa  hiyo  kwa  urahisi  tunalitumia  hilo  neno,  lakini
‘Dharma’ ndio  hasa  neno  linalofaa  zaidi kwa  vile  lina  maana  pana  zaidi  kuliko
neno ‘dini.

Enyi  bhikkhu  (watawa),  Dharma  pamoja  na  kanuni  zinazofundishwa  na  Budha
zinatoa  mwangaza  mkubwa  sana.  Hizi  kanuni  hazifuatwi  kisirisiri.  Hizi kaninu ni
dhahiri  kabisa  kama  jua  au  mwezi. Zaidi ya   haya , kuhusu  Dharma  inayofundishwa
na Budha  hakuna  ‘mkono  uliokunjwa  wa  mwalimu’.  Hii  ina  maana  kwamba  Budha  kama  mwalimu  hakuweka  siri  katika  mafundisho  yake.  Na  kwa  ajili  hiyo  hakuna
siri  au  mafumbo  katika  Ubudha  ambazo  zinatakiwa  kukubalika  tu  bila  swali  lolote
na  mfuasi,  kwa  imani  tu  kama  kipofu.

 Budha  alikuwa   akisema mara kwa mara kwamba  yeye  hana  siri  katika  kufundisha
kwake.  Anafundisha  mambo  yote  anayoyafahamu.  Ile  tabia  ya  mwalimu kufahamu
jambo,  lakini  bado  halifundishi,  anawaachia  walimu wengine.  Yaani,tabia ambayo
mwalimu   hafundishi  kila  kitu  anachokifahamu,kwa  sababu yoyote ile,  lakini  siyo
kwa vile mwalimu  hafahamu  analotakiwa  kufundisha,  hii  haikuwa  tabia  ya  Budha.
Dharma   ndio  ukweli wa  juu  kabisa  ambao  umefundishwa  na  Budha.  Ni  njia
tukufu   ya  maisha   ambayo  wakati  wote  inatusaidia  na  kutudumisha  juu  na
haituruhusu  tushuke  katika  hali  nyingine  za  mateso  kama  vile  motoni,  au  maisha
ya    kinyama    au    maisha    ya    ahera,    kama    mashetani    au    kama    viumbe    wengine  
ambao  hawajabahatika.  Kwa  hiyo  kama  tukiifuata  Dharma,  Dharma  itatuhifadhi  na
kutusaidia  kikamilifu,  haitaruhusu  tuteseke  katika  hali  zozote  za  mikosi.
Hii  ndiyo  maana  ya  neno  Dharma  katika  ubudha.  kwa  vile  ubudha  siyo  dini  ya
ufunuo,  Budha hakupata  habari  zozote  kutoka  mbinguni  kwa  sababu  hakuwa  na
mwalimu  yoyote  wa  kumfundisha  kuufikia  mwangaza,  Alichofanya  ni  kutumia
juhudi  yake  yote,  kuyaondoa  kabisa  mawazo  maovu,  maneno  maovu  na  matendo
maovu,  na  kwa  kupalilia  tabia  zote  njema,  kwa  kuitakasaa  akili  yake,  hatimaye
alifikia  utakaso  na  umakini  wa  akili  kiasi  kwamba  alielewa  kikamilifu  jinsi  kila
sehemu  ya  mbingu  inavyofanyo  kazi.  Hii  ndio  tunaita  kuufikia  mwangaza.
Ubudha  ni  matokeo  ya  juhudi  za  mtu  mkubwa  aliyejitolea  maisha  yake  na  muda
wake  kutafuta  ukweli  wa  juu.  Lazima  tueleze  tuna  maana  gani  tunaposema  ukweli
wa  juu . Kwa  sababu  watu  wengi  wanadai  kwamba  wanaufahamu  ukweli.,lakini
hakuna  mapatano  kati  yao  kuhusu huo ukweli. Wabudha  wanamaanisha  nini
wanapolitumia  neno  hili?  Tunajua  kwamba  zipo  kweli  za  aina  nyingi.  Lakini  siyo
zote  zinaweza  kuitwa  ukweli  wa  juu.  Kweli  fulani  zinaweza  kuwa  sahihi  kwa
kipindi  fulani,lakini  baadaye,  kwa  ajili  ya  mabadiliko  katika  hali  halisi,  hazibakii
kuwa  kweli.  Ukweli  ambao  umefahamika  na  kuhubiriwa  na  Budha  ni  ukweli  wa
juu,  kwa  sababu  hakuna  mtu  yoyote  anayeweza  kuupinga  usahihi  wa  neno  hata
moja  alilozungumza,  hata  akitumia  uchambuzi  wa  kisayansi.  Ni  ukweli  wa  juu
kwa  sababu  unadumu  milele  na  hauwezi  kubadilika  kufuatana  na  muda  au  hali
yoyote.  Imani  nyingine  nyingi  zilizoonekana  kwamba  ni  kweli  hapo  mwanzo
imebidi  zirekebishwe  kufuatia  maendeleo  katika  ugunduzi  wa  sayansi Mafundisho
ya  Budha  pekee  ndio  hayajapingwa,  na  pia  yanathibitishwa  na  ugunduzi  mpya wa
sayansi.  Maadili  aliyoyafundisha  Budha  kwa  msingi  wa  ukweli  wa  juu.  pia  ni
halali  ingawa  yametokea  maendeleo  makubwa.  katika  ustaarabu (civilization).

Wabudha  hawana  sababu  ya  kujieleza  upya  kuhusu mada  kama  vile   
☯  Euthanasia -  kumuua  mtu anayeishi  kwa  kutumia  mashine 
☯  Mercy  killing -  kuua  kwa  huruma 
☯  Birth  control -  uzazi  wa  majira 
☯  Pre-marital  sex – kujamiiana  kabla  ya  ndoa ☯  Animal  rights – haki  za  wanyama 
☯  Environment nk             mazingara 


KWA  NINI  DINI  INAHITAJIKA
Tukizumgumza  kwa  ujumla  ni  lazima  tukubali  kwamba  dini.  zote  zimeleta  faida
fulani,  ingawa  wasomi  wengine  kama  Bertand  Russell  wanasema  dini  imewaletea
binadamu  madhara  zaidi  ya  wema.  Kuhusu  fitina,  chuki  na  ubaguzi  kama
zinavyoelezwa  na  wana  dini  tofauti  anasema ‘  Wale  wasiokuwa  na   dini  wanaishi
kwa  amani  bila  kupigana  na  kubishana.  Wale  ambao  wana   dini  mara  nyingi
wanapigana  kwa  sababu  ya  imani  zao  tofauti  za  dini ‘ Lakini  sio  wote
watakubaliana  na  yeye.

Kila  dini  kubwa  ,  kama  ni  Ukristu,  Ubudha,   Uislamu  au  Uhindu  imewasaidia
sana  binadamu.  Kama  binadamu  wameweza  kutenda  maovu  ingawa  kuna  dini.,  je
ingekuwa  ni  maovu gani ambayo  yangeweza  kutokea  kama  wangekuwa  hawana  dini
ya  kuiamini. Kama  kwa  mfano  serikali  za   dunia  zikitangaza  kwamba  sheria
hazitashinikizwa kwa  muda  wa  saa  24,  muda huo  unaweza  kutosha  kulianganiza
kabisa  taifa.  Na  kama  dini  isipokuwepo  kuwathibiti  binadamu  tatizo  hilo  litakuwa
kubwa  zaidi.  Kwa  hiyo  hatuwezi  kuilaumu  dini  kwa  tabia  ya  binadamu.
Lazima  tuongeze  hapa  kwamba  wapo  watu  wastaarabu  ambao  ni  wema  katika  asili
yao  na  hawahitaji  uthibiti  unaoletwa  na  watu  wa  dini.  Budha  alisema  kwamba
mafundisho  ya  dini  yanapaswa  kuonekana   kama  raft  ya  kumsaidia  mtu  kufika
ng’ambo  ya  pili.  Mtu  akifikia  kiwango  cha  juu  cha  maendeleo  ya  kiroho,  hahitaji
mwongozo  tena,  anaishi  maisha  ya  kufuata  maadili . Wengi  wetu  tunaihitaji  rafti,
misingi  ya  kidini  kutusaidia  kuishi  kwa  maadili  na  kukamilika  kiroho.

MISINGI  YA  KIDINI  NI  MUHIMU
Kama  binadamu  tunao wajibu  wa  kudumisha  misingi  fulani  mizuri  kwa  faida  yetu  na  wengine,  Hii
inaleta  maana  nzuri,  kwa  sababu  tunapofuata  kanuni,  pia  tunawalinda  wengine.  Kama  sisi
hatujakamilika, ikiwa  tunataka kuishi vyema na jirani ,  lazima  tuhakikishe  kuwa  tuna  uzio  ,  ama  sivyo
kutatokea  ubishi,  vurugu  na  kutoelewana.  Ttukijenga  uzio     au  ukuta,  sio  tu  tunailinda  nyumba
yetu  na  familia  yetu,  lakini  pia  tunazilinda  nyumba  za  jirani  zetu.  Kwa  hiyo  kufuata kanuni  ni
sawa  na  hivi. Tunapoamua  hatutaua  au  kuwadhuru  wengine , basi  tunawaruhusu  wengine  kuishi  kwa
amani  bila  woga.  Huu  ni  wema  mkubwa  sana  tunaowafanyia  wengine.  Tunapaswa  kuacha
kuwatapeli  na  kuwadhulumu  wengine  ili  waweze  kuishi  kwa  amani  bila  kutuogopa  au  kutushuku.
Kama  tunafahamu  jinsi  ya  kutimiza  wajibu  wetu, tunadumisha  hadhi  yetu  ya  kibinadamu  pamoja
na  akili  yetu,  kwa  kufanya  hivyo  tunadumisha  amani,  muafaka  na  shwari  katika  maisha  yetu.
Lakini  kama  Robert  Frost  anavyosema  katika  shain  lake  zuri  ‘ Kutengeneza  Ukuta’   kama  sisi  ni
wema  kwa  asili,  na  jirani  zetu  ni wema  kwa  asili,  basi  uzio  hazitahitajika.  Jamii  zingine  za  kale
ambazo  zinaitwa  hazijaendelea  zilikuwa  zikiishi  namna  hiyo.  Lakini  sisi,  hasa  tunapoishi  mijini,
tunahitaji  uzio  za  dini  kujilinda  wenyewe pamoja  na kuwalinda wengine.

Ili  kufanya  hivi  tunapaswa  kuzifuatwa  kanuni  za  dini (sila)  sila  ina  maana  nidhamu  ya  kuizoeza
akili.  Tunajizoeza  kwa  kuifuata  misingi  fulani  ya  dini  kwa  kuona  hatani  iliyopo  katika  kuipuuzia.
Kuna  tofauti  katika  kanuni  za  kibudha  na  amri  au  sheria  za  kidini  za  imani  nyingine.  Watu  wengi  wanayatii  majukumu  yao  ya  kidini  kwa  kuogopa  kuadhibiwa.  Inawezekana  kabisa  bila  kutishiwa
kwenda motoni , watu  wengi  wangezipuuzia  sheria  zao  za  kidini.

Ipo  njia  yenye  sehemu  mbili  ya  kufuata  wakati  wa  kuzitii  sila  au  kanuni.  Tunapoacha  kuua  kwa
kuelewa    kwamba    tutawafanyia    ukatili    na    mateso    viumbe    wengine,    hiyo    inaitwa    Varitta    Sila.
Kuacha  kufanya  uovu (kuepuka,  kujizuia ).   Wakati  huo  huo  tukikuza  wema,  huruma,  maelewano,
hiyo  inaitwa  Caritta  Sila. Kutenda  wema  (matendo  ya  wema).  Hivi  vipengele  viwili  vya  thawabu
viendelezwe,  vya  kujizuia  kufanya  uovu  na  kutenda  matendo  mema.

Isipokuwepo  adhabu,  watu  wataichukua  fursa  hiyo  kutenda  matendo  maovu  bila
kuonyesha  huruma  yoyote.  Katika  Ubudha  kuzIngatia  sila  au  kanuni  kuna  maana;
‘Naizoeza  akili  yangu  iache  kufanya  mambo  fulani  yenye  madhara,  siyo  kwa  ajili
ya  mungu  au  kuogopa  adhabu  yake,  isipokuwa  kwa  kuelewa  kwamba  hayo  ni
makosa.  Siogopi  adhabu  au  kutegemea  zawadi,  lakini  nafanya hivyo kwa  vile
ndivyo  ninavyotakiwa  kufanya,  kwa  sababu  inaleta  faida  kwa  wengine  na  kwangu.’
Budha  amesema; ‘ Nawashauri  kutokana  na  uzoefu  wangu.  Siyo  habari  ambazo
nimeshushiwa  kutoka  juu.  Nimefanya  matendo  mabaya  nilipozaliwa  karne  zilizopita
na  nakumbuka  jinsi  ilivyobidi  niteseke  kwa  ajili  ya  makosa  hayo.  Ndio  maana
nawaambia  ni  bora  muache  kutenda  matendo  mabaya  ili  muepushe  mateso.  Pia
nimefanya  matendo  mema  mengi  nilipozaliwa  karne  zilizopita,  na  naweza  kuelewa
maisha  mazuri,  ya  amani  na  fanaka  niliyoishi  kwa  ajili  ya  hayo  matendo  mazuri.
Kwa  hiyo  nawashauri  ninyi  pia  mtende  matendo  mazuri  ili  mpate  matokeo  hayo
hayo  mazuri.  Kama  unataka  kufahamu  zaidi  kuhusu  hili  somo,  soma  hadithi  za
Jataka  ambazo  zinaelezea  kuhusu  Budha  katika  maisha  yaliyopita.

Katika  Ubudha  hatuwezi  kukuta  amri,  dogma,  sheria  za  dini  au  vitisho  vya
adhabu  ya  kidini.  Dini  kazi yake siyo  kawaadhibu  watu  ila  kuwashauri  watu  la
kufanya  na  lile  ambalo  siyo  la  kufanya.  Ukifanya  tendo  lolote   la  kiovu,
utakumbana  na  matokeo  yake.   Siyo  Budha  au  dini  itakayokuadhibu.  Kitendo
chako  mwenyewe  ndicho  kinachokutengenezea  mbingu  yako  au  moto.  Mwingine
hawezi  kufanya  hivyo.

Kama  nilivyosema  mwanzo  hata   watu  wa   kale  walikuwa  na  maadili  katika  nafsi
zao  na  walikuwa  wanaweza  kutofautisha  kati  ya  sahihi  na  siyo  sahihi.  Lakini
jamii  zilivyoendelea  hizi  hisia  za  asili   ziliendelezwa  na  kutengenezwa  kuwa
kanuni  za  tabia  kudumisha  sheria  na  usalama.  Kuhakikisha  kwamba  hizi  zitafuatwa
viongozi  wakasema  kwamba  zimethibitishwa  na  mungu  pamoja  na  zawadi  au
adhabu  za  milele.   Kwa njia  hii,  tunaweza  kusema  kwamba dini zimewasaidia
binadamu.

FAIDA  YA  KUTOSHEKA
Siku  moja  mfalme  fulani  alimwendea  Budha  na  kumuuliza  swali. ‘ Ninapowatazama
wafuasi  wako  naona shwari,  uchangamfu  na  ngozi  inayong’ara. Pia  nimesikia
kwamba  wanakula  mlo  mmoja  tu  kwa  siku,  lakini  kwa  kweli  nashindwa  kuelewa
wanaweza  vipi  kuudumisha  mwenendo  huu  wa  maisha.’  Budha  akampa  jibu  zuri’ “
Wafuasi  wangu  hawayajutii  matendo  waliyoyafanya  zamani  isipokuwa  wanajitahidi  zaidi  na  zaidi  kutenda  matendo  mema.  Siyo  kwa  kujuta,  kusali  na  kuabudu
isipokuwa  kwa  kuwasaidia  wengine  ndio  watu  wanaweza  kufanya  toba  kwa
makosa  waliyoyafanya  zamani.  Wafuasi  wangu  hawana  wasiwasi  kuhusu  mambo
yatakayowafika  baadaye.  Wanatosheka  na  chochote  wanachopata  na  kwa  hiyo
wanadumu  katika  hali  ya  kutosheka.  Hawawezi  kamwe  kusema  hiki  au  kile
hakiwatoshi.  Huo  ndio  mtindo  wa  maisha  yao  kwa  hiyo  wanaweza  kuidumisha
shwari,  uchangamfu  na  kung’ara  ngozi  kwa  ajili  ya  huko  kutosheka.”
Mtu  yoyote  anaweza  kuudumisha  huu  uchangamfu  kwa  kutosheka.  Kama  mtu
akiuliza  kwa  nini  hatuna furaha katika  maisha  yetu  ingawa  vitu  tulivyo  navyo  ni
zaidi ya  mahitaji  yetu,  ni  njia  gani  sahihi  ya  kumjibu ?  Jibu  sahihi  ni,  kwa  sababu
hatutosheki  ,’  Kama  tungetosheka,  tusingesema  kwamba  hiki  au  kile  ni  pungufu.
Hatuwezi  kutosheka  kwa  ajili  kuna upinzani  kati  ya  hamu  zetu  za  kibinafsi
ambazo  hazina  kikomo  na  sheria  ya  kutodumu  kwa  vitu (anicca )

Moja  kati  ya  ushauri  mzuri  uliotolewea na  Budha  kwetu  sisi  ili  tuuzingatie  kama
msingi  ni “ Kutosheka  ndio  utajiri  mkubwa  kuliko  yote,’  Mtu  tajiri  haina  maana
kwamba  anacho  kila  kitu,  mtu  tajiri  kila  wakati  anahofia  kuhusu  uhai  wake.  Kila
wakati    yupo    katika    hali    ya    woga    na    wasiwasi,    akifikiria    kwamba    watu
wanasububiri  kumdhuru  au  kumdhulumu.  Tajiri  hawezi  kutoka  nje  bila  mlinzi,  na
ingawa  anayo  milango mingi  ya  chuma  na  kufuli  katika  nyumba  yake,  hawezi
kulala  bila  woga na  mashaka.

Kwa  kulinganisha naye,   mtu  aliyetosheka  ni  mtu  mwenye  bahati  sana  kwa  sababu
akili    yake    imeepushwa    na    usumbufu    wowote    wa    aina    hiyo.    Yeye    ndiye    tajiri
kweli.  Kwa  hiyo  kutosheka  ni  nini?  Wakati  mtu  anapofikiria  ‘Kiasi  hiki  kinatosha
kwangu  mimi  na  familia  yangu,  na  sihitaji  zaidi  ya  hivi ‘ huko  ndiko  kutosheka.
Kama  kila  mtu  akifikiria  namna  hii,  basi  hayawezi  kuwepo  matatizo  yoyote.
Tukidumisha  kutosheka   kwa  namna  hii,  husuda  haiwezi  kuivuruga  akili  yetu  na
kwa  hiyo  tutawaruhusu  watu  wengine   wastarehe  katika  maisha  yao.  Kama  hakuna
husuda,  hasira  pia  haiwezi  kutokea,  kutakuwa   hakuna  dhuluma  na  umwagaji  damu
na  kila  mtu  kwa  hiyo  ataishi  kwa  amani.

Maisha  ya   kutosheka  daima  yanampa  mtu  matumaini  na  imani  Hii  siyo  ndoto  ya
mchana.  Kwa  karne  25 watawa  wa  kIbudha  wameishi  maisha  haya  ya  amani
katika  maskani  zao.  Na  walei  wengi  wa  Kibudha  pia  wameishi  maisha  ya
kutosheka  bila  kuruhusu  tamaa  za  kuvuka  mahitaji  yao  ya  msingi.  Ni  ajabu  sana
jinsi  ambavyo  tunahitaji  vitu  kidogo  sana  kutosheka.  Fikiria  kuhusu  jambo  hili.

 JIFUNZE  KUKABILIANA  NA  MATATIZO  YA   MAISHA
Kwa  sababu    ya  tamaa    za    kibinafsi,    tunataka    tuishi    maisha    ambayo    daima
hayabadiliki,  ya  amani  na  fanaka  bila  kujali  kwamba  vitu  vilivyopo  mbele  yetu
havidumu.  Kwa  hiyo  tamaa  zetu  za  kibinafsi  haziwewi  kutoshelezwa  kwa sababu
kila kitu  hakidumu.  Mabadiliko  ndio  kawaida  ya  mbingu  yote.  Hakuna  kitu
kinabakia  vilevile,  na  tunahukumiwa  kuwania  vitu  ambavyo  daima  vipo  nje  ya
ulingo  wetu – kwa sababu  sisi  na  hivyo  vitu  vinabadilika  mara tu  vinapoguswa.
Lakini  bila  kujali  mabadiliko  hayo,  tunasukumwa  na  kuhadaika,  na  tamaa  za
ubinafsi,  bado  tunawania  maisha  ambayo  hayabadiliki

Siku  moja  Budha  alimshauri Ananda;  kama mtu  yoyote  akiuliza  swali  kwa  nini
kifo  kinatokea,  itabidi  uwaambie kinatokea  kwa  sababu  watu  wanazaliwa,  kama
hakuna  anayezaliwa  kutakuwa hakuna  kifo.  Kama  ukitaka  kukizuia  kifo  kwa nguvu,
basi  huyajui  maumbile Na  ukifanya  hivyo  utakuwa  unaenda  kinyume  na  sheria  za
maumbile.

Watu    kwa    ujumla      wanapenda    uzazi    lakini    wanaogopa    sana    kuoza    na    kufa.
Machweo  ya   jua  katika  nchi  moja  ni  mawio  ya  jua  katika  nchi  nyingine,  kwa
jInsi  hiyo  hiyo, kifo  siyo  mwisho  wa  maisha,  kwa  vile  kifo ni  mwanzo  wa  maisha
mengine.  Kuzaliwa  kiumbe  ndio  mwanzo  wa  kifo.  Kifo  ndio  mwanzo  wa  maisha
Kuzaliwa  kunaleta  cheti  cha  kifo  kwa  hiyo  tukitaka  kuepusha  kifo,  inabidi
tuepushe  watu  kuzaliwa.

Kwa  hiyo  tunapaswa  kuwa  na  hekima  na  kuacha  kurudia  makosa  yetu  na  tujitaya
rishe  kwa  maisha  ambayo  yatakuwa  hayana  mateso.
Tukichunguza  kwa  makini  tunaweza  kuelewa  kwa  nini  dunia imejaa  dhuluma  na
uonevu.  Tunaanza  kuona  kwamba  hiyo  siyo  kazi ya  muumbaji  kigeugeu  bali
inatokana  na  matendo  yetu  mema  au  mabaya  ya  zamani. (karma )  tunaweza  kuona
taathira  ya  matendo  yetu  mema  au  mabaya  hata  katika  maisha  haya,  ukitenda
mema  yanakufika  mema,  ukitenda  mabaya  yanakufika  mabaya.     Hakuna mtu yeyote kati ya wale wanaoishi kwa thawabu haiamini sheria hii ya
karma,kama yeye ni Mbudha au hata kama hana dini. Na wote,isipokuwa wachache tu
,kati ya wale wanaoishi kiovu,hawaamini katika karma.Kwa sababu mambo yao kila
wakati ni ya kufuru.,kwa vile wanasema,”Tule na tunywe kwa sababu kesho
tutakufa”Kuongea namna hii ni ishara ya kuendekeza starehe kupita kiasi.Hizi falsafa za
kula na kunywa kumbe ndiyo chanzo cha misemo ya kuipinga Dharma

UBUDHA  KWA  WALEI
Maisha  ya  kidunia  yana  matatizo  sana.  Kwa  hiyo  siyo  rahisi  kwa  walei  kuishi
maisha ya  dini.  Wakijaribu  kuishi  maisha  ya  dini  kwa  kubadilisha  tabia  zao  hii
inaweza  kuleta   usumbufu kwa  watu  ambao  wanaishi  miongoni  mwao.  Watu  wa
familia  yao  au  rafiki  watashindwa  kuyaelewa  haya  maisha  yao  mapya;. Lakini
wakiyabadilisha  maisha  yao  polepole  wengine  wanaweza  kujirekebisha  na  kwenda
nao  sambamba.

Kwa  upande  mwingine,  mtu  anaweza  kuishi  maisha  ya  dini  bila  kuwasumbua
wengine  kwa  kuwa  na  upole,  uaminifu,  subira,  uvumilivu,  umoja,  maelewano  na
ufahamu.   Lakini  hata  hapo  pia,  hizi  tabia  nzuri  zinaweza  kuleta  matatizo iwapo
wengine  watataka  kukudhuru  kwa  ajili  ya  upole  wako  Siyo  lazima  uwe  na
thawabu  kupita  kiasi. ili uishi  maishi  ya  dini   kwa  walei.  Jaribu  tu  kuishi  maisha
ya  kawaida.

Budha  alianzisha  hii  njia  ya  kuishi  inayofaa kwa walei  kwa  ajili  ya  matatizo
waliyo  nayo,  Walei  hawatakiwi  kuwaiga  watawa.  Na  watawa  hawatakiwi  kuwaiga
walei. Leo  hii,  utaona  watawa  wengine  wanaishi  kama  walei,  na  walei  wengine
wanaishi  kama  watawa.

Kwa  kutambua  ugumu  unaowafika  katika  kutimiza  majukumu  yao  ambayo  inabidi
wayatimize  ili  wazitunze  familia  zao,  watu  inawabidi  wafanye  mambo  fulani.
Budha  alisema  wanaweza  kupata  furaha  ya  aina  nne;-  kwa  kuchuma  hela  na
kuziwekeza(investing),  kwa  kustarehe  kiasi  katika  anasa  za  dunia  kwa  kutumia
fedha  ambazo  wamezipata  kihalali,  kwa  kuepusha  madeni  kwa  kuhakikisha
kwamba  hela  zao  wanazitumia  vizuri,  na  kwa  kuishi  maisha  ya  thawabu  ,watu
wakielewa  kwamba  hawajamfanyia  ubaya  mtu  yoyote  ,wanakuwa  hawana  sababu
ya  kujisikia  vibaya.  Hisia  hii  ya  raha  ndio  furaha  kubwa  kuliko  zote  anazoweza
kuhisi  mtu .  Furaha  zote  nyingine  zisizokuwa  na  maana  zitatoweka  akilini  mbele
ya  furaha  hii .
 
Hii  hali  ya  furaha ambayo  wanaidumisha  na  kuibakiza  katika  akili , itabaki  nao
mpaka  siku  ya  kufa  na  itawasaidia  kupata  maisha  mazuri  watakapozaliwa  tena .
Kwa  sababu  wataondoka  duniani  na  akili  ambayo  haijachanganyikiwa . Hivi  ndivyo
watu  wanavyotakiwa  kurekebisha maisha  yao  ikiwa  wanataka  kuishi  maisha  ya
kidunia  kwa  faida.  Tofauti  na  walei  , wapo  watu  wachache  ambao  kwa hiari  yao
wanaamua  kuyaacha  kabisa  maisha  ya  kidunia  na  kuwa  watawa . Watu  hawa
wanakuwa  na  amani  ya  aina  tofauti  kabisa .


KUWA  NA  AKLI  YA  WAZI  KATIKA  UBUDHA
         
Upali  ,mfuasi  tajiri  sana  wa  dini  nyingine ,  wakati  fulani  alikuja  kumuona  Budha
na  kumwambia  kwamba  alitaka  kuwa  mfuasi  wake.  Budha  alimuuliza, “ Kwa  nini
unataka  kuwa mfuasi  wangu? “ Upali  akajibu ,  “Watu  wanasema  kwamba
mafundisho  yako  ni  mazuri’  Budha halafu  akauliza,  “Umeshayasikia  mafundisho
yangu  yoyote ?”  Upali  aliposema  bado  ,swali  la  Budha  lililofuatia  lilikuwa “ ,Sasa
unajuaje  kama  utaweza  kuyafuata  mafundisho  yangu  au  la;  Hiyo  siyo  njia  ya  mtu
kubadili  dini  yake ,Mtu  ni  lazima  ajifunze  na  ajaribu  kuyaelewa  mafundisho  kabla
hajaamini .”

Hapo  Upali  akawa  na  dhamira  zaidi  ya  kumfuata  Budha  na  akasema  “Muadhama,
nadhani  huu   ushauri  wako  unatosha  kabisa  kwa  mimi  kuelewa  mafundisho  yako
yalivyo.  Ingekuwa  nimemfuata  kiongozi  wa  dini  nyingine , angenipokea  na
angetangaza  kwamba  mtu  fulani  pia  amekuwa  mfuasi  wa  dini  yake.  Lakini  badala
yake  muhashamu,  wewe  unanishauri  kuisoma  na  kuamua  kama  nataka kuyafuata
haya  mafundisho.”

Budha  alipotaka  kuhubiri ,  hakuhubiri  kama  vile  anataka  kutoa  hotuba
hadharani.Alichunguza  akili  na  uwezo  wa  kufahamu  wa  wasikilizaji  wake.  Na
aliwashauri  kufuatana  na uwezo  wa  akili   yao  kushika  mambo  ili  waweze
kuyaelewa  mafundisho  yake  kwa  urahisi.

JINSI  YA KUMUONA  BUDHA .
Mmoja  wa   wafuasi  wa  Budha   aliyekuwa  akiitwa  Vakkali  alikuwa  na  tabia  ya
kumtazama  Budha  kila  siku,  kuutazama  mwili  wake.  Budha  alipogundua  hili
akamwuliza,  “ Unafanya  nini  hapa?  Jibu  lake  Vakkali lilikuwa “
Muadhama  ,  ninapovitazama  viungo  vyako  vilivyo  shwari , na  ngozi  yako
inayong’ara  najisikia  vizuri  sana.”  Baada  ya  hapo  Budha  akamwuliza,  “Unategemea
kupata  faida  gani  kwa  kupendezewa  na  mwili  ambao  ni  mchafu ,  unanuka , wenye
sura    mbaya,    na    usiodumu?    Mtu    anayeiona    Dharma,    anamuona    Budha.    Hii
inakusaidia  kumuelewa  Budha  wa  kweli.  Kama  unachotaka  ni  kumuona  Budha  wa
kweli.,  basi  unapaswa  kumuunda  Budha  huyo  katika  akili  yako  kwa  kupitia
mafundisho  yake.,

Tunayatazama  maisha  yetu  visivyo, Tunaiona  miili  yetu  kama  ndio  maisha
yenyewe.  Hatulitazami  hili  swala  kwa  usahihi.  Nguvu  za  akili  na  maisha  yetu
vyote  vinafanya  kazi    pamoja.  Mwili  ni  nyumba  tu  ya  roho  zetu.  Tunayatumia
maisha  yetu  yote  kuutunza,  kuulisha,  kuuosha,  kuupendezesha  mwili  wetu,  kwa
kutumia  hela  nyingi,  bila  kuelewa  kwamba  miili  yetu  inaleta  matatizo  mengi  na
mateso.

MISINGI  MITATU  MUHIMU  KATIKA  UBUDHANidhamu  [sila],kuiendeleza  akili  [samadhi],na  kupata  hekima,  ndio  misingi  mitatu
ya  maisha  ya  binadamu.  Binadamu  tu  ndio  wanaweza  kuziendeleza  hizi  tabia
nzuri.  Lengo  kubwa  katika  hii  misingi  mitatu  ya  Ubudha  ni  kuzifuata  kanuni
[sila].
SILA.
Mtu  ni  kiumbe  ambaye  anaishi  katika  jamii  na  anaendeleza  tabia yake  kwa
kuhusiana  na jamii  anayoishi,  kwa  hiyo  kila  analolifanya  linaleta  taathira  sio  tu
kwake  lakini  pia  katika  jamii  yake. Kuzingatia  maadili  pia  kutaleta  taathira.
Maadili  yanajumuisha  thawabu  zote  za  watu  wa  heshima.  Inalinganishwa  na
thawabu  kwa  ujumla,  na  mambo  mengi  yanayostahili  sifa  yametafsiriwa   kuhusiana
na  malengo  ya  kujitakasa  na  kujizuia ,  katika  matendo,  maneno  na  mawazo  ya
mtu. Kwa kawaida sila inaeleweka  kumaanisha  kanuni  tano  za  maadili  ambazo  ndizo
sheria  za mlei.  Wanatakiwa  kuanza  safari  yao  ya  kiroho  kwa  kuzifuata  hizi  kanuni
tano,  na  kila  mlei  anategemewa  kuzifuata  hizi  kanuni za msingi.
Na pia kufuatana na mwenendo wa Ubuddha hizi lazima zifuatwe kwa kuzingatia uzoefu
na mantiki. Lengo la mwisho la Ubuddha linavuka dhana hii,lakini wakati wote mtu
lazima aishi kwa uhusiano na mambo ya dunia hii, na kwa kuzifuata kanuni hizi tano,
Wabudha wanaishi kwa kuzingatia hali halisi ya dunia hii .Binadamu amegundua kwa
kutumia utashi wake pamoja na manitiki kwamba akiifuata njia fulani,anaweza kufaidika
yeye pamoja na dunia nzima.Kwa hiyo anatumia utashi wake kuifuata hiyo njia. Huku
ndiko kuutambua ubinadamu wa mtu kutambua uwezo wake na wajibu.

Sila au maadili maana yake ni kwamba lazima tujifunze kuishi kama watu ambao
hawaleti madhara,watu wapole. Tunatakiwa kuishi bila kuivuruga amani na furaha ya
wengine.Tukiweza kufanya hivi itakuwa mafanikio makubwa sana. Nidhamu,tabia
njema,kanuni na maadili yanalingana na hili neno ‘Sila,’huu ndio msingi wa kuanza
maisha ambayo ni ya kidini.

Kama nyumba ikijengwa bila kuweka msingi mzuri,haitakuwa imara.Mtu wa kisasa
amegundua baada ya kutaabika sana jinsi ambavyo ni muhimu sana kuishi maisha ya
‘Sila’ Ina maana kuheshimu haki ya watu wengine kuishi.Kama tukiamini kwamba dunia
ilitengenezwa kwa ajili yetu peke yetu, basi tutachukua kila kitu kilichopo bilka kujali;
Hatutajali litakalowafika viumbe wengine, hatutajali mazingira kama vile mimea,mito,
anga, na kadhalika. Mwisho wake kwa sababu ya dosari za ekolojia zilizosababishwa na
maisha  yetu ya kisasa tutajiangamiza wenyewe.Mbudha mzuri anaheshimu na anajali
wanavyoishi viumbe wengine,

Budha, kwa upeo wake mkubwa alifahamu kwamba hatuwezi kukamilika mara
moja.Kwa hiyo anaanza kwa kuituhimiza tuache kutenda matendo yenye madhara.
Tukipata maendeleo katika kuweka msingi mzuri wa maadili,tunaweza kuanza kuitakasa
akili.Ubudha unamruhusu mtu kujiendeleza kufuatana na kiwango chake cha ufahamu na
haimwekei mtu kanuni ngumu za kufuata bila kujali uwezo wake au mtazamo wake wa
maisha.  Kanuni zina faida kwa kukuza tabia za kiutu na thawabu.Hizi ni tabia ambazo ni muhimu
sana kudumisha amani na furaha. Hizi kanuni zinatakiwa kufuatwa sio kwa kuogopa
adhabu lakini kwa ajili ya hekima na huruma. Budha alipotushauri, “Tusifanye
uovu,”ilikuwa ni kwa faida ya watu wengine.

Kama binadamu, ni wajibu kuwasaidia wengine kwa kutenda ukarimu,kwa wema,na
kuwapa msaada wengine wanaohitaji msaada wetu kuondoa mambo
yanayowasibu,mashaka na matatizo mengine.Kwa kutoa msaada kwa wengine bila
ubinafsi, sio tu tunawasaidia wengine,bali pia tunaupunguza ubinafsi wetu. Tusifanye
tendo jema huku tukiwa na hila moyoni,kwa sababu tendo letu zuri litaharibiwa na
ubinafsi na hizo dhamira mbaya.

Kwa hiyo maana halisi ya dhana ya Kibudha ya ‘kuacha kutenda uovu’ na ‘kutenda
mema’haitegemei adhabu au zawadi,isipokuwa lengo lake ni kuzipunguza tabia zetu za
ubinafsi ili tuongeze usafi wa mawazo.Hatutumii vitisho kuwafanya watu wazingatie
kanuni.Kutumia vitisho badala ya kuwaelewesha watu hakutawafanya watu wawe na
hisia ya huruma, na badala yake unawezakuwafanya watu wawe washirikina au wawe
watu wanaotii kauli bila kuuliza maswali.

Kuepuka uovu na kutenda mema,ni mambo mazuri sana,lakini hayatoshi.Kutokana na
uzoefu tunafahamu kwamba ikiwa bado uchu,hasira na kuduwaa kumejichimbia sana
ndani ya akili, bado tutakuwa tunaweza kutenda matendo mabaya kwa hiyo ipo haja
kwetu sisi kuitakasa akili. Kufanya hivi itabidi tuilinde akili yetu na tuyaondoe mawazo
yoyote yale ambayo ni machafu. Iwapo mawazo na dhamira chafu zitazimwa,akili daima
itakuwa safi na yenye wema, na tutakuwa tumelifikia lengo letu la mwisho.

Lakini kama binadamu,tunafahamu kwamba maisha yetu tunayoishi siyo ya kwanza na
ya mwisho. Faida ya kuwa binadamu ni kwamba tunalifahamu hili na tunaweza
kujitayarisha kwa maisha ya baada ya kifo. Watu wengi wanatumaini kwenda mbinguni
baada ya kifo lakini tunavyoona jinsi dini zingine wanavyoielezea tunalazimika kufikia
uamuzi kwamba hawajui ni kitu gani au iko wapi au ufanye nini ili uzipate starehe za
mbinguni? Hata unavyoishi hapa duniani unaweza kuzipata starehe za mbinguni. Wakati
tajiri fulani alipouliza ushauri wa Budha jinsi ya kwenda mbinguni baada ya kifo,Budha
alimjibu, “Wewe ni tajiri. na bado unauliza ufanye nini ili uzipate starehe za mbinguni?
Kwa nini unataka usubiri mpaka utakapokufa ndipo uzipate starehe za mbinguni?Hata
unapoishi hapa duniani unaweza kuzipata starehe za mbinguni kama utayatumia maisha
haya vizuri.. “

Budha alikuwa mwalimu mzuri wa dini ambaye hakutaka kuingiza ushirikina ,vishawishi
au woga katika maisha ya watu.Watu lazima wajifunze jinsi ya kuyatumia haya maisha
vizuri,wajue jinsi ya kuepuka matatizo,vurugu,migogoro,mashaka na karaha,ili wapate
elimu zaidi na hekima.Baada ya kuiendeleza hekima,wataweza kuyarekebisha maisha
yao.


FURAHA YA MWILI NA YA AKILI
Ingawa vurugu nyingine haziwezi kuwa dhahiri kwetu, mawazo fulani ya kiovu
yaliyojichimbia sana katika akili yanaweza kuwepo.Wakati fulani tunaweza kuwa
kimya,na kuwa na sura ambayo haijakunjamana kwa vile hakipo kitu chochote
kinachotsumbua; lakini kama vurugu fulani ikitokea,hali yetu inabadilika tunakuwa na
ghadhabu na sura yetu inakunjamana. Ile furaha ya mwili ambayo kwa muda inatokea
katika akili tunaidhania kwa makosa kuwa ndio furaha ya kweli.Lakini sio hasa furaha ya
kweli. Furaha ya mwili ni kutosheka tu kwa hisia. Tabia ya furaha ya mwili ni kwamba
inatoweka baada ya muda kidogo Kutafuta furaha ya mwili kusifananishwe na kutafuta
furaha ya akili. Furaha ya mwili haidumu, inapiga chenga nyingi,na baada ya kuondoka
inakuwa chachu. Pia, inaweza kuwa na gharama, ingawa hairidhishi, lakini furaha ya
kweli sio hivyo,yenyewe hainunuliwi,inatoka katika chanzo cha ndani ya akili, na
inadumu muda mrefu.

Starehe ya mwili tunayoipata wakati huu inatuhadaa kwa sababu haidumu. Wakati huo
huo, hatuwezi kuwa na furaha kwa kudumisha hitilafu za mawazo kama vile
woga,hasira,husuda, uhasama na nia ya kudhuru. Wakati hayo mambo hayapo akilini,
basi ule uangavu unaotokea kwa muda katika akili ndio tunaita furaha.


FURAHA INATOKANA NA MATENDO MEMA.
Ili kuwa na furaha tunatakiwa kutenda matendo mema zaidi na zaidi.Maana ya matendo
mema ni kutoa msaada fulani kwa wengine ili kuyaondoa mateso yao. Furaha
tunayoipata kwa kutenda mema ni muhimu kuliko kulimbikiza mali.Kila tunapofanya
tendo jema kwa imani na ufahamu,tunapata furaha na tunajisikia vizuri.Hii ndio tunaiita
thawabu. Hali ya akili tunavyoiendeleza katika maisha haya inaamua maisha tutakayoishi
baada ya kufa.Baada ya kufa hakuna kitu chochote kinachoweza kutusaidia isipokuwa
thawabu au karma.Kwa hiyo lazima tujitahidi kwa kadiri tuwezavyo kufanya wema
katika maisha haya kwa sababu ndio pekee bima yetu ya kuhakikisha kwamba tunazaliwa
upya katika maisha ya bahati.

Wapo watu fulani wasiokuwa na ufahamu ambao wanaweka vitu vya thamani katika
jeneza kwa kufikiria kwamba itamsaidia mtu aliyekufa. Lazima tuitumie akili yetu na
tuelewe mambo bila tu kufuata tabia za kizamani za waliotutangulia. Muda umefika wa
kuziacha tabia hizi ili tusilaumiwe na watu wa dini nyingine ambao watafikiria hizi ni
tabia za Kibudha.Budha kwa mfano hakuwataka wafuasi wachome kitu chochote kwa
ajili ya watu waliokufa. Alitushauri kuzichoma moto takataka za akilini.

2. SAMADHI KWA KUPITIA KUTAFAKARI
Samadhi ndio msingi wa pili, kuyakusanya mawazo au kuiendeleza akili ili kupata amani
na shwari kwa kuidumisha akili ili ifikirie mada moja tu.Akili za watu ambao hawana
uzoefu kama huu ni dhaifu sana. Akili zao ni dhaifu kwa sababu woga unawasumbua.
Tunazo hisia za kujiona kwamba hatuko salama,kwamba hatuna kinga ya kutosha,na kwa
ajili ya huo udhaifu tunajishuku.Kila dakika, nguvu zetu za akili zinapotea bila faida yoyote, kwa kupitia hisia zetu tano. Hizi hisia zetu tano zinaitoa nje nishati ya nguvu yetu
ya akili, na zinazitumia hizo nguvu kukaribisha vitu ambavyo vinatuletea wasiwasi, woga
na mashaka.  Wakati huo huo vinaweza kuunda kinachoonekana kuwa ni kuridhika kwa
hisia au msisimko, Hatimaye kwa njia hii, tunaivuruga akili. Tunakusanya vitu visivyofaa
kutoka nje kupitia hizi hisia tano, na tunaichanganya  akili yetu. Kwa hiyo akili inakuwa
haina muda wa kupumzika na inakuwa dhaifu kwa ajili ya huku kupotea kwa nguvu. Ni
kama maporomoko ya maji ambayo yanaendelea kutiririka na kueneza maji kila pahali
kwa sababu hakuna njia nzuri ya kuyaongoza maji yatumike vizuri. Lakini boma inaweza
kujengwa kutengeneza umeme ambao unaweza kutumika kwa kazi tofauti nzuri.

Injinia , baada ya kuona kwamba kuna hasara kubwa ya maji yanayoporomoka anaamua
kujenga boma kuyavuna hayo maji na kutengeneza umeme unaotokana na nguvu ya maji,
ili kuliangaza bonde lote. Kwa njia hii hii, tunapoteza nguvu zetu kwa vile hatayakusanyi
mawazo yetu. Budha alitushauri tusizipoteze nguvu zetu kwa kupitia hizi hisia tano,
isipokuwa tuipumzishe akili, ili isilazimike kufanya uamuzi kila wakati kutokana na
habari zinazotokana na hisia hizi tano. Ni usumbufu, mkubwa sana kwa akili  Katika kile
kipindi cha kupumzika kwa akili, tunaweza kufikiria mada moja tu, bila kuiruhusu akili
kuirukia mada hii au ile.na kwa hivyo tutaweza kuiendeleza   akili yetu. ‘Bhavana”
maana yake kuiendeleza akili, yaani kufanya akili ikusanye  na kuivuna nguvu

inayopotea na ijiumbe upya.Akili ikikua kikamilifu,inakuwa na nguvu kubwa,na woga
wote,wasiwasi wote,na hisia zote za kujiona uko hatarini zitatoweka.Halafu utakuwa na
ujasiri,elimu na hekima. Ili tudumishe maadili,lazima tutafakari,ambayo ndiyo
inaitwa’samadhi’ Samadhi ni hali ambayo akili inakuwa shwari. Akili ambayo
haijanidhamishwa ina tabia ya kwenda huku na huku na siyo rahisi kuimiliki na inaweza
kufuata wazo au taaswira yenye madhara makubwa  Ili kuizuia hii tabia mbaya ya akili,
mawazo ni lazima yakusanywe ili akili  ifikirie mada moja tu,

     Na baada ya muda,pole pole akili inaweza kudumu katika mada moja.,kama
inavyoelekezwa.Kwa kuchagua mada fulani,inawezekana kuuondoa udhaifu fulani wa
akili.Kutafakari siyo kuifikiria mada yoyote maalum, Kutafakari ni kuiweka wazi akili ili
iweze kufikiria mada moja.Lakini kwa kufikiria mada fulani unaweza kuuondoa udhaifu
fulani,Kwa mfano ukitafakari kuhusu urafiki,unaweza kuyaondoa makali ya
uadui,gadhabu na husuda.Ukitafakari kuhusu sehemu za mwili ambazo ni chafu au zenye
magonjwa,unaweza kuiondoa tabia ya ngono.Ukitafakari kwamba siku moja
utakufa,labda utachangamka na kufanya kazi kwa bidii,na hutaridhika na mafanikio
uliyoyapata.Ukizitafakari tabia nzuri za Budha,unaweza kuondoa kukata tamaa ya
maisha,wasiwasi na mawazo ya kutojiamini.Kwa kukuza huruma,mtu anayasahau
matatizo yake mwenyewe  na anaona kwamba wapo watu wengi wenye matatizo.
Kwa kuendelea na mazoezi ya kutafakari Budha na wafuasi wake waliweza kupata
uwezo mkubwa wa akili. Waliweza kuondoa kabisa uchu,chuki na kuzumbaa.Iwapo
tunataka furaha tujifunze jinsi ya kuipumzisha akili na kuiendeleza na kuzing’oa kutoka
kwenye mizizi yake nguvu za uovu zilizomo ndani.

  Wakati ule tunapotafakari,tunakuwa na amani lakini mara tu tunapoacha kutafakari na
kurudia katika hali yetu ya kawaida ya kufikiri,amani na furaha vinatoweka,na vurugu inarudi.Maji katika dimbwi yanaweza kufunikwa na majani mengi juu,lakini kule chini
maji ni masafi,ukiyasogeza majani kwa mkono,utayaona maji masafi chini,lakini
ukiuondoa mkono wako majani yatarudi.Kutafakari kunasaidia kuyaonyesha’maji masafi
ya akili’Mwangaza kamili ni wakati  ambapo majani yanaondoka moja kwa moja.,na
maji yanakuwa masafi moja kwa moja.

    Tunapotafakari akili yetu inatakasika.Hii ni kwa sababu hatuyaruhusu mawazo maovu
kuiviruga akili yetu..Kwa njia hiyo hiyo,tunapoacha kutafakari,mawazo maovu yanaanza
tena.

  Tukiyafunika na ndoo majani ya kijani kwa muda wa wiki tatu halafu tuyafunue
tena,tutaona yamebadilika rangi. kwa ajili ya kukosa mwangaza wa jua Na
tunapotafakari,mabadiliko mengi yanatokea katika akili.Tunakuwa shwari bila hasira
yoyote kwa sababu akili yetu inakuwa katika taathira nzuri ya mkusanyiko wa
mawazo.Lakini tukiirudia tena hali yetu ya kawaida ya maisha,mawazo yale yasiyofaa
yanarudi,kama vile yale majani yanapofunikwa yanabadilika rangi kwa sababu
mwangaza wa jua haupiti.Kwa hiyo upo umuhimu wa kuiendeleza akili ili isirudie katika
hali ya kuchanganyikiwa.Lengo la kutafakari ni kukusaidia kuiwezesha akili daima
ibakie katika hali ya kutakasika.

ELIMU NA HEKIMA
Hekima sio elimu.Tunapata elimu baada ya kusikiliza,kusoma,na kuyaangalia mambo
mengi katika dunia hii,lakini sio hekima hasa.Hekima inatokea katika akili wakati
vipingamizi vya akili,vizuizi na vikwazo vingine vinapoondoshwa. .Kuna wasomi wengi
duniani ambao,bila shaka,wanayo elimu nzuri lakini kwa bahati mbaya hawana hekima
sahihi.

   Watu wengi wana akili lakini vitendo vyao havina mantiki,kwa sababu wana hasira za
karibu,wana maringo,wana hisia  zinazolipuka upesi,wana uchu,wana hisia
zinazobadilika mara kwa mara.Kwa upande mwingine,kuna watu wengine ni wapole,na
ingawa wana subira,uvumilivu na tabia nyingine nyingi nzuri,hekima yao siyo nzuri na
wanaweza kupotoshwa kwa urahisi na wengine.Tukiwa na ukarimu bila
hekima,tutajiletea matatizo kwa sababu watu wengine watakuwa wanatuomba hela kila
wakati.Kwa hiyo hekima na thawabu lazima viwe pamoja.

KUWA HURU KWA KUTUMIA HEKIMA
Panna..Hekima ni hatua ya tatu na ya mwisho katika njia.Baada ya kuzingatia
maadili,mfuasi anajifunza kutafakari.Mawazo yake yanapokusanyika,anakuwa na uwezo
wa kuelewa jinsi vitu vilivyo hasa.Hekima ni kuielewa dunia vyema kwamba
haidumu,hairidhishi na siyo ya kukumbatiwa.Elimu ni aina  tatu,a)ile inayopatikana
kutokana na kujifunza,b)ile inayopatikana kwa kufikiri,c)ile inayopatikana kwa
kutafakari.Hii ya mwisho ndiyo kilele.Inamwezesha mtu kuifikia nirvana.

     Kuzumbaa,ujinga,na mawazo maovu yanapotoka akilini,uangavu unatokea badili
yake.Huu uangavu ndiyo hekima.Kila tunapozidi kujifunza mambo ya kidunia na akili
iliyozubaa,ujinga wetu unaongezeka.Akili ikifunguka kikamilifu maendeleo yanaweza kutokea,na hapo  tu ndipo hekima na  na ufahamu na utakaso vinatokea katika akili.Haya
ndiyo maendeleo ya ndani.

      Hatuwezi kuuleta huu uangavu,utakaso na ufahamu kutoka nje.Ni lazima utoke ndani
.Sila,Samadhi.,Panna-mazoezi haya ya akili ndiyo misingi mitatu mikuu ya Kibudha ya
kuizoeza akili. Maendelezo zaidi ya akili kwa madhumuni ya kupata ukamilisho yanaitwa
Adhi Sila. Shwari ya akili inaitwa Adhi Citta(Samadhi).Kupata hekima ya juu kwa
kuendeleza ufahamu kunaitwa Vipassana.,ambayo pia inaitwa Adhi Panna.Kwa hiyo,hii
ndiyo misingi mitatu mikubwa ya Ubudha ya kuizoeza akili,

MPANGO WA MAFUNZO WA MISINGI MITATU
Huu ndio mpango wa kufundisha maadili Kibudha,kwa kutumia misingi mitatu
inayotegemeana.Nazo ni sila,ambazo ni kanuni za maadili ambazo zinafuatwa kwa
makusudi na kwa hiari kubadili tabia za maneno na matendo,samadhi,kufundisha
mkusanyiko wa mawazo,na panna,kuendeleza hekima ili maadili yaweze kukamilika.Sila
ndiyo inaaminika ambapo yale mengine mawili yanajengwa. Mpango wa njia
unaonyesha kuwa Ubudha  ni kitu abacho kinatekelezeka.Kukamilika kwa sila
kunatambulika kuwa ndio msingi wa kazi yote ya kiroho.Mtu mwenye akili anatakiwa
ajizatiti katika sila,.aiendeleze akili yake(citta),na aendeleze hekima(panna).Mtu kama
huyo anaweza kujinasua kutoka kwenye nyavu za uovu.
http://deniceshonko.blogspot.com/2012/04/makala.html
http://deniceshonko.blogspot.com/

2 comments:

  1. Kazi Bomba sana. Ama kweli, Hekima sio elimu.Tunapata elimu baada ya kusikiliza,kusoma,na kuyaangalia mambo
    mengi katika dunia hii,lakini sio hekima hasa.Hekima inatokea katika akili wakati
    vipingamizi vya akili,vizuizi na vikwazo vingine vinapoondoshwa. .Kuna wasomi wengi
    duniani ambao,bila shaka,wanayo elimu nzuri lakini kwa bahati mbaya hawana hekima
    sahihi.

    ReplyDelete
  2. Hakuna nishati ambayo inaweza kulingana na akili ya binadamu, Akili ndio
    mtangulizi wa kila kitu, akili ndio inayoongoza na vitu vyote vinavyo chanzo
    chake katika akili.. Budha amesema , ‘ Siifahamu nishati nyingine kubwa kuliko
    akili ya binadamu ambayo inaweza kukimbia mbio sana,. Kwa mfano wale ambao
    wamesoma sayansi wanaweza kuelewa mara moja umbile la atom. Atom
    inabadilika mara milioni chache katika muda wa nukta moja.

    ReplyDelete