Mwanaume mmoja kipofu wa nchini Uingereza ameweza kumuona mkewe kwa mara ya kwanza baada ya kufanyiwa upasuaji wa macho ambapo jino lake la juu lilipandikizwa kwenye jicho lake. Mjenzi Martin Jones, 42, alipata upofu wa macho yake yote mawili zaidi ya miaka 10 iliyopita baada ya bomba la madini ya aluminium yaliyokuwa yamechemka kumpasukia usoni, liliripoti gazeti la Daily Mail la Uingereza.













