Menyu

Kiswahili

Utamaduni mpya ulijitokeza uliokuwa Kiafrika na Kiislamu ukajielewa kuwa sehemu ya dunia ya Uislamu.

SWAHILI HUB

BLOGU YA KISWAHILI KWA AJILI YA KUSAFISHA FIKRA ZA WAAFRIKA!

DUNIYA MTI MKAVU

Kiumbe siulemee kamwe... Likuondokealo, lina heri nawe.

CHINI YA SHAMSHI

Mjomba'ngu Shamshi Kuzaliwa kwangu kulifululizwa na majonzi yas’o kuwa na mfano. Hili si ada kwa wana wengi duniani. Na kama ilivyokuwa kawaida katika jamii za kwetu Raha, waliniona mwenye shari hivyo kunipa jina Tabu. Japo haya si kuyanga’mua papo kwa hapo, niliyafahamu mtuo kwa mtuo kadri miaka ilivyozidi kuporomok...

Said Ahmed Mohammed

Uamuzi wa kuchagua hadithi zilizoandikwa kwa Kiengereza kufasiriwa kwa Kiswahili, ulitokana na Macmillan wenyewe. Nao walizichagua hadithi hizo kwa ubora wa hadithi zenyewe na umaarufu wa waandishi wenyewe.

Swahili Hub

Sababu ya Ndoa Nyingi Kuvunjika



Sababu ya ndoa nyingi kuvunjika kwa wingi ni mabadiliko mengi ya kimaisha tunayoishi sasa kulinganisha na zamani. Baadhi ya hizo ni:

Kupungua kwa wake kutegemea waume zao kimaisha. Katika mfumo wa maisha wa zamani, asilimia kubwa ya wanawake walikuwa wanategemea waume zao kwa chakula, mavazi n.k 100% Katika familia nyingi, baba pekee ndiye aliyekuwa anatengeneza fedha. Hilo lilipelekea wake kuwa wavumilivu wa matatizo katika ndoa zaidi ya siku hizi sababu walikua wakihofia wataishi vipi bila mume ilhali hawana kipato chochote. Siku hizi mashosti wengi wanatengeneza fedha zao wenyewe. Wakichoka wanajiondokea tu. Suala hili pia lilichangia sababu ya pili hapa chini

Pastor Michael Njoroge na Kahaba



Ama kweli siku za kiama zinukiapo, dalili wazo hudhihirika. Mambo yanayotukia siku hizi hata mfano mwafaka hamna. Ajabu iliyoje kumwona kasisi Michael Njoroge akiwatumia mahawara ili kukudhi mahitaji yake binafsi?

Wanaume nao Kutumia Sindano za Kupangilia Uzazi


Baada ya wanawake kwa miaka mingi kuwa ndio wenye jukumu la kutumia vidonge na njia nyingine katika kupangilia uzazi, watafiti nchini China wamekamilisha utafiti wao ambao utawasaidia wanaume kuwasaidia wanawake jukumu hilo baada ya kutoa sindano kwaajili ya wanaume zitakazosimamisha uzalishaji wa mbegu za kiume kwa muda Wanasayansi nchini China wamekamilisha utafiti wao wa sindano kwaajili ya wanaume ili kusaidia kuzuia mimba zisizohitajika.

Siri Wazi?


Swahili Hub

Diamond asema alikumkuta Wema Sepetu kitandani kama alivyozaliwa na rafiki yake

Naseeb Abdul Jumaa a.k.a Diamond

Naseeb Abdul Jumaa a.k.a Diamond amezungumza mambo makubwa juu ya uhusiano wake wa kimapenzi na Wema Isaac Sepetu.

Visa vya mapenzi


Swahili hub

Afisa mipango wa halmashauri ya Chamwino, mkoani Dodoma, bwana Fred Kaombwe (34) amejiua kwa kujifyatulia risasi mwenyewe kutokana na wivu wa kimapenzi juu ya mke wake.

Vijana Katika Maisha ya Ndoa


Kwa heshima na taadhima nachukua nafasi hii kukukaribisha mpenzi msikilizaji katika makala ya vijana kutoka viunga vya Radio Vatican. Bila shaka utakumbuka kuwa majuma machache yaliyopita tulitafakari suala la wito kwa wanadamu wote kuwa watakatifu (Rejea, Walawi 19) na namna mbalimbali za kuishi wito huo zikiwa ni pamoja na ndoa, ukasisi na kujiweka wakfu kama mtawa wa kiume au wa kike. Leo, napenda kuufungua moyo na mawazo yako kuitazama nafasi ya ndoa katika jamii na hali za familia kwenye dunia ya utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Elimu Kwenye Mtandao


Swahilihub

Na Mtemi Zombwe
KAMA inawezekana kwa bibi aliyeko kijijini kabisa kupokea fedha kwa njia ya mtandao kupitia simu yake ya mkononi,  vivyo hivyo inawezekana kabisa kwa mwanafunzi wa shule au chuo kusoma bila kuwa na karatasi  wala mwalimu. Ni teknolojia ya habari na mawasiliano iliyozaa elimu kwa njia ya mtandao.

UTENGANO


“Mimi sitakubali hilo lifanyike hata kidogo humu nyumbani. Heri nimwondokee kuliko kuwa na mke mwenza.” Nilisikia sauti ya mama ikija juu. Baba naye aliguruma kwa sauti akimwarifu mama kuwa ni wajibu wake kumrithi huyo mjane na kuwa hakuna kitakachomzuia. Majibizano hayo makali baina yao yalinifanya kuingiwa na wasiwasi. Nilikuwa sebuleni nikifanya marudio ya mwishomwisho kwa matayarisho ya mtihani wa kitaifa. Runinga nayo ilionyesha pasi na wa kuitazama.

Je Wajua Kwamba…


Kuna mambo mawili ukizaliwa na kuishi yatakuhusu
Ni ama wewe utazaliwa mwanaume au mwanamke
Kama wewe utazaliwa mwanamke uko salama,
Lakini kama wewe utazaliwa mwanaume kuna mambo mawili yatakuhusu