Sababu ya ndoa nyingi kuvunjika kwa wingi ni mabadiliko mengi ya kimaisha tunayoishi sasa kulinganisha na zamani. Baadhi ya hizo ni:
Kupungua kwa wake kutegemea waume zao kimaisha. Katika mfumo wa maisha wa zamani, asilimia kubwa ya wanawake walikuwa wanategemea waume zao kwa chakula, mavazi n.k 100% Katika familia nyingi, baba pekee ndiye aliyekuwa anatengeneza fedha. Hilo lilipelekea wake kuwa wavumilivu wa matatizo katika ndoa zaidi ya siku hizi sababu walikua wakihofia wataishi vipi bila mume ilhali hawana kipato chochote. Siku hizi mashosti wengi wanatengeneza fedha zao wenyewe. Wakichoka wanajiondokea tu. Suala hili pia lilichangia sababu ya pili hapa chini













