Menyu

Kiswahili

Utamaduni mpya ulijitokeza uliokuwa Kiafrika na Kiislamu ukajielewa kuwa sehemu ya dunia ya Uislamu.

SWAHILI HUB

BLOGU YA KISWAHILI KWA AJILI YA KUSAFISHA FIKRA ZA WAAFRIKA!

DUNIYA MTI MKAVU

Kiumbe siulemee kamwe... Likuondokealo, lina heri nawe.

CHINI YA SHAMSHI

Mjomba'ngu Shamshi Kuzaliwa kwangu kulifululizwa na majonzi yas’o kuwa na mfano. Hili si ada kwa wana wengi duniani. Na kama ilivyokuwa kawaida katika jamii za kwetu Raha, waliniona mwenye shari hivyo kunipa jina Tabu. Japo haya si kuyanga’mua papo kwa hapo, niliyafahamu mtuo kwa mtuo kadri miaka ilivyozidi kuporomok...

Said Ahmed Mohammed

Uamuzi wa kuchagua hadithi zilizoandikwa kwa Kiengereza kufasiriwa kwa Kiswahili, ulitokana na Macmillan wenyewe. Nao walizichagua hadithi hizo kwa ubora wa hadithi zenyewe na umaarufu wa waandishi wenyewe.

Swahili Hub

MWANDISHI ADAM SHAFI


MWANDISHI ADAM SHAFI

Nimepokea simu. Simu ya maana. Adam Shafi yuko Majuu. Kaja kikazi Uholanzi. Yeye mtaalamu wa lugha ya Kiswahili. Baada ya kumaliza kapitia Uingereza katika mji mmoja wenye wakazi wengi wa Kitanzania, yaani Milton Keynes. Ni wastani wa saa moja kwa treni toka London.  Mrefu, mchangamfu, mzungumzaji aliyesheheni “mastore” kibao. Nishakutana na waandishi wa kila sampuli. Wanaojificha: wakimya, wasioongea sana, wapole wanaokaa chumbani kati kati ya watu ukadhani hawapo. Wanaopiga kelele, wakijafaragua; ama wenye aibu…

Shaaban Robert


Maisha
Shaaban Robert alizaliwa tarehe 1 Januari, 1909 kijiji cha Vibambani jirani na Machui kilomita 10 kusini mwa mji wa Tanga, alipata elimu yake katika shule ya Msimbazi, jijini Dar-es-salaam kati ya miaka 1922 na 1926 alifaulu na kupata cheti. Akaajiriwa na serikali ya kikoloni akawa karani katika idara ya forodha huko Pangani mwaka 1926 – 1944. Bila shaka kukaa kwake miaka mingi hivi katika mji wa kihistoria uliokuwa mahali pa utamaduni wa Kiswahili tena mahali patulivu kumesaidia maendeleo yake Shaaban kama mwandishi wa Kiswahili.

Lugha ni Njia


UTANGULIZI
Lugha imewahi kufafanuliwa kwa jumla kama mfumo wa sauti za nasibu za kusemwa zinazotumiwa na watu wa jamii Fulani wenye utamaduni unaofanana kwa madhumuni ya mawasiliano katika jamii hiyo.
Wataalamu wengi wa isimu (sayansi ya kuchanganua lugha na kuieleza jamii) kamusi ya kiswahili sanifu TUKI 1981 oxford press uk. 86 na lugha wanaelekea kukubaliana kwamba lugha ni mfumo wa sauti nasibu ambazo hutumiwa na jamii kwa madhumini ya mawasiliano kati yao ( massam ba D.P.B na wenzake 1999, TUKI).

Malenga wa Mvita Ahmad Nassir


AHMAD NASSIR ni mzee mswahili wa Mombasa. Kwa upande wa babake ni Mtangana na kwa mamake ni Mkilindini. Hizi ni miongoni mwa kabila za asili ya Kiswahili za ki-mvita, yaani MombasaBwana Ahmad alizaliwa kuze, Mombasa mnamo 1936. Kama watoto wengine wa kimombasa wa wakati huo aliingia chuoni kusoma kuraani na dini ya kiislamu. Mafunzo hayo aliyapata kwa babu yake Sheikh Muhammad Ahmad Matano, mpaka alipohitimu.

PENDO LA SIRI. [23/05/2012]


PENDO LA SIRI.
[23/05/2012]
Hayo ya hayawi hayawi, yaliniangukia kama nanga. Kiza kilichojimwaya kati ya upenyu wa mwanga katika aushi yangu. Yapo niliyoyaamini; Anenae kuwa pendo, si faida ni uvundo. Huyo yu katika mwendo, wa ujinga na ubaya. Na'mi kwa ari ambayo sikufahamu mwanzo wake, nikatii amri yakuwa tupendaneni, tusitendeyane ubaya...

Ama kwa hakika yalianza kama mchezo. Mara 'My son', mara wavutia mara sijui nini:- almuradi niliungulika na mengine kuyatia asali bandia. Nikajitia upofu kwa dhana kuwa mapenzi ya mtandaoni

Jifunze Fasihi


Fasihi kama dhana, imeelezwa na wengi kwa kuegemea nadharia na mitizamo
mbali mbali.  Hata hivyo ni muhimu tufahamu ya kwamba maana inayopewa dhana au
kitu fulani, huwa inachukuana na matumizi ya dhana yenyewe, watu wanaohusika,
mahali dhana hiyo inamotokea, na hata kipindi au wakati husika.  Hii ndiyo sababu
twapata maana mbalimbali zikitolewa kuhusu fasihi.  Kwa mfano, waandishi wengi wa
Kimagharibi wamesisitiza kwamba fasihi yahusu tu kazi zilizoandikwa.

Lugha Tukufu ya Kiswahili


Historia ya Kiswahili

Maeneo penye wasemaji wa Kiswahili
Historia ya Kiswahili imeanza takriban miaka 1000 iliyopita kwenye pwani la Afrika ya Mashariki.
Neno Swahili ni neno la asili ya Kiarabu Sahil lenye maana ya pwani; sawahil ’’as-sawāhilī’’ (السواحلي) ni wingi wake kwa kumaanisha yote yanayohusiana na pwani, watu au utamaduni wa eneo la pwani.
Yaliyomo  [ficha]
1 Mwanzo katika miji ya pwani
2 Lugha ya biashara
3 Kiswahili wakati wa ukoloni
4 Kiswahili leo
Lugha ni?

Wanamziki


Mwanamuziki wa kike wa nyimbo za kiinjili.

Rose Muhando ambaye hujulikana pia kwa jina la Rose Muhando;amezaliwa mwaka 1976 katika kijiji cha Dumila, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, nchini Tanzania) ni msanii maarufu wa muziki wa injili katika lugha ya swahili katika kanda ya Afrika Mashariki.

Waandishi Mashuhuri wa Vitabu


Said Ahmed Mohammed



Uamuzi wa kuchagua hadithi zilizoandikwa kwa Kiengereza kufasiriwa kwa Kiswahili, ulitokana na Macmillan wenyewe. Nao walizichagua hadithi hizo kwa ubora wa hadithi zenyewe na umaarufu wa waandishi wenyewe. Hadithi zilizochaguliwa ni Tropical Fish (Samaki wa Nchi za Joto) iliyoandikwa na Doreen Baingana kutoka Uganda, The Madman (Kichaa) iliyoandikwa na Chinua Achebe kutoka Naijeria, na In the Cutting of a Drink (Katika Kutiliwa Kinwaji) iliyoandikwa na Ama Ata Aidoo kutoka Ghana. Hadithi ya Muhammed Said Abdulla” Mke Wangu” ambayo ni hadithi ya zamani sana iliazimwa kutoka katika kitabu fulani cha Rüdder Köpper Verlag ambayo iliwaruhusu kuichapisha katika mkusanyo wetu.